Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Matokeo ya utafutaji

Mwa 2:24 (SUV)

Kwa hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja.

Efe 5:33 (SUV)

Lakini kila mtu ampende mke wake kama nafsi yake mwenyewe; wala mke asikose kumstahi mumewe.

Efe 5:25 (SUV)

Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake;

Efe 5:22 (SUV)

Enyi wake, watiini waume zenu kama kumtii Bwana wetu.

Efe 5:23 (SUV)

Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe, kama Kristo naye ni kichwa cha Kanisa; naye ni mwokozi wa mwili.

Efe 5:28 (SUV)

Vivyo hivyo imewapasa waume nao kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe. Ampendaye mkewe hujipenda mwenyewe.

Mit 18:22 (SUV)

Apataye mke apata kitu chema; Naye ajipatia kibali kwa BWANA.

Mt 19:4 (SUV)

Akajibu, akawaambia, Hamkusoma ya kwamba yeye aliyewaumba mwanzo, aliwaumba mtu mume na mtu mke,

Mt 19:5 (SUV)

akasema, Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja?

Mt 19:6 (SUV)

Hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi aliowaunganisha Mungu, mwanadamu asiwatenganishe.

Mk 10:8 (SUV)

na hao wawili watakuwa mwili mmoja; hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja.

Mk 10:9 (SUV)

Basi alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe.

Ebr 13:4 (SUV)

Ndoa na iheshimiwe na watu wote, na malazi yawe safi; kwa maana waasherati na wazinzi Mungu atawahukumia adhabu.

Rum 7:2 (SUV)

Kwa maana mwanamke aliye na mume amefungwa na sheria kwa yule mume wakati anapokuwa yu hai; bali akifa yule mume, amefunguliwa ile sheria ya mume.

Kum 23:2 (SUV)

Mwana wa haramu asiingie katika mkutano wa BWANA; hata kizazi cha kumi asiingie aliye wake katika mkutano wa BWANA.

Kum 22:13 (SUV)

Mtu akitwaa mke, akamwingilia na kumchukia,

2 Nya 18:1 (SUV)

Basi, Yehoshafati alikuwa na mali na heshima tele, tena akafanya ujamaa na Ahabu.

Kut 21:10 (SUV)

Kwamba ajitwalia mke mwingine, chakula chake huyo, na nguo zake, na ngono yake, hatampunguzia.

1 Fal 1:4 (SUV)

Naye kijana huyo alikuwa mzuri sana; akamtunza mfalme, akamtumikia; walakini mfalme hakumjua.

Rum 7:3 (SUV)

Basi wakati awapo hai mumewe, kama akiwa na mume mwingine huitwa mzinzi. Ila mumewe akifa, amekuwa huru, hafungwi na sheria hiyo, hata yeye si mzinzi, ajapoolewa na mume mwingine.

Mwa 29:27 (SUV)

timiza siku zake saba, nasi tutakupa huyu naye kwa utumishi utakaonitumikia, miaka saba mingine.

Mal 2:14 (SUV)

Lakini ninyi mwasema, Ni kwa sababu gani? Ni kwa sababu BWANA amekuwa shahidi kati ya wewe na mke wa ujana wako, uliyemtenda mambo ya hiana, angawa yeye ni mwenzako, na mke wa agano lako.

Hes 31:17 (SUV)

Basi kwa ajili hiyo mwueni kila mume katika hao watoto, na kila mwanamke aliyemjua mume kwa kulala pamoja naye.

Mwa 29:28 (SUV)

Yakobo akafanya hivi, akatimiza siku zake saba. Naye akampa Raheli binti yake kuwa mkewe.

1 Kor 7:3 (SUV)

Mume na ampe mkewe haki yake, na vivyo hivyo mke na ampe mumewe haki yake.