Soma Biblia Kila Siku 8Mfano

Uliyebatizwa na kumkubali Yesu kuwa Mwokozi wako, jua hakika kuwa Yesu Kristo anakuombea kwa Mungu Baba mbinguni!Kristo Yesu ndiye aliyekufa; naam, na zaidi ya hayo, amefufuka katika wafu, naye yuko mkono wa kuume wa Mungu; tena ndiye anayetuombea (Rum 8:34). Hutuombea nini? Somo la leo latupa jibu. Anatuombea ulinzi. Tutalindwa kwa kuliitia jina la Yesu Kristo. Mungu atulinde na nini? Atulinde na mafarakano. Yaani Wakristo tuwe na umoja (m.11: Baba mtakatifu, kwa jina lako ulilonipa uwalinde hawa, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo). Pili atulinde na yule mwovu, yaani Shetani (m.15: Mimi siombi kwamba uwatoe katika ulimwengu; bali uwalinde na yule mwovu). Halafu anatuombea utakaso. Uwatakase kwa ile kweli; neno lako ndiyo kweli (m.17).
Andiko
Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 8 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu kila siku hasa katika kitabu cha Matendo ya Mitume, Kumbukumbu la Torati, na Yohana pamoja na maelezo yatakayokusaidia kutafakari na kuelewa Neno la Mungu kwa urahisi.
More
Tunapenda kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabiblia.or.tz
Mipangilio yanayo husiana

Soma Biblia Kila Siku 12

Soma Biblia Kila Siku 9

MWANGA Kuvutiwa Maishani Na Mwanga Ajabu Wa Mungu

Soma Biblia Kila Siku 06/2020

BibleProject | Safari ya Kujifunza Kutoka Luka Na Matendo

Soma Biblia Kila Siku Aprili 2021

Soma Biblia Kila Siku Machi 2021

Soma Biblia Kila Siku 10

Soma Biblia Kila Siku 11
