Methali 24:15-18
Methali 24:15-18 Biblia Habari Njema (BHN)
Usivizie kama mwovu kushambulia makao ya mtu mwema, wala usijaribu kuiharibu nyumba yake, maana mtu mwema huanguka mara nyingi lakini huinuka, lakini mtu mwovu huangamizwa na janga. Usishangilie kuanguka kwa adui yako; usifurahie moyoni mwako kujikwaa kwake, maana Mwenyezi-Mungu aonaye hayo hatapendezwa; huenda akaacha kumwadhibu.
Methali 24:15-18 Swahili Revised Union Version (SRUV)
Ewe mtu mbaya, usiyavizie makao yake mwenye haki; Wala usipaharibu mahali pake pa kupumzika; Kwa maana mwenye haki huanguka mara saba akaondoka tena; Bali wasio haki hukwazwa na mabaya. Usifurahi, adui yako aangukapo; Wala moyo wako usishangilie ajikwaapo; BWANA asije akaliona hilo, likamkasirisha; Akageuzia mbali naye hasira yake.
Methali 24:15-18 Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia (SUV)
Ewe mtu mbaya, usiyavizie makao yake mwenye haki; Wala usipaharibu mahali pake pa kupumzika; Kwa maana mwenye haki huanguka mara saba akaondoka tena; Bali wasio haki hukwazwa na mabaya. Usifurahi, adui yako aangukapo; Wala moyo wako usishangilie ajikwaapo; BWANA asije akaliona hilo, likamkasirisha; Akageuzia mbali naye hasira yake.
Methali 24:15-18 Neno: Bibilia Takatifu 2025 (NENO)
Usivizie kama haramia afanyavyo ili kuyashambulia makao ya mwenye haki, wala usiyavamie makazi yake, kwa maana ingawa mtu mwenye haki huanguka mara saba, huinuka tena; lakini waovu huangushwa chini na maafa. Usitazame kwa kufurahia adui yako aangukapo; wakati anapojikwaa, usiruhusu moyo wako ushangilie. BWANA asije akaona na kuchukia akaiondoa ghadhabu yake mbali naye.