Methali 23:19-22
Methali 23:19-22 Biblia Habari Njema (BHN)
Sikia mwanangu, uwe na hekima; fikiria sana jinsi unavyoishi. Usiwe mmoja wa walevi wa divai, wala walafi wenye kupenda nyama, maana walevi na walafi wataishia kuwa maskini, anayetumia siku yake kusinzia atavaa matambara. Msikilize baba yako aliyekuzaa, wala usimdharau mama yako akizeeka.
Methali 23:19-22 Swahili Revised Union Version (SRUV)
Sikia, mwanangu, uwe na hekima, Na kuuongoza moyo wako katika njia njema. Usiwe miongoni mwao wanywao mvinyo; Miongoni mwao walao nyama kwa pupa. Kwa maana mlevi na mlafi huingia umaskini, Na utepetevu humvika mtu nguo mbovu. Msikilize baba yako aliyekuzaa, Wala usimdharau mama yako akiwa mzee.
Methali 23:19-22 Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia (SUV)
Sikia, mwanangu, uwe na hekima, Na kuuongoza moyo wako katika njia njema. Usiwe miongoni mwao wanywao mvinyo; Miongoni mwao walao nyama kwa pupa. Kwa maana mlevi na mlafi huingia umaskini, Na utepetevu humvika mtu nguo mbovu. Msikilize baba yako aliyekuzaa, Wala usimdharau mama yako akiwa mzee.
Methali 23:19-22 Neno: Bibilia Takatifu 2025 (NENO)
Sikiliza, mwanangu na uwe na hekima, weka moyo wako kwenye njia iliyo sawa. Usiwe miongoni mwa wanywao mvinyo, au wale walao nyama kwa pupa, kwa maana walevi na walafi huwa maskini, nako kusinzia huwavika matambara. Msikilize baba yako, aliyekuzaa, wala usimdharau mama yako atakapokuwa mzee.