Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 146

146
Sifa kwa Mungu Mwokozi
1Msifuni Mwenyezi-Mungu!
Umsifu Mwenyezi-Mungu, ee nafsi yangu!
2Nitamsifu Mwenyezi-Mungu maisha yangu yote;
nitamwimbia Mungu wangu muda wote niishipo.
3Msiwategemee wakuu wa dunia;
hao ni binadamu tu, hawawezi kuokoa.
4Binadamu akitoa pumzi yake ya mwisho,
anarudi mavumbini alimotoka;
na hapo mipango yake yote hutoweka.
5Heri mtu anayesaidiwa na Mungu wa Yakobo,
mtu aliyeweka tumaini lake kwa Mwenyezi-Mungu, Mungu wake,
6 # Taz Mate 4:24; 14:15 aliyeumba mbingu na dunia,
bahari na vyote vilivyomo.
Yeye hushika ahadi yake milele.
7Yeye huwapatia wanaoonewa haki zao,
huwapa wenye njaa chakula.
Mwenyezi-Mungu huwapa wafungwa uhuru,
8huwafungua macho vipofu.
Mwenyezi-Mungu huwainua waliokandamizwa;
huwapenda watu walio waadilifu.
9Mwenyezi-Mungu huwalinda wageni,
huwategemeza wajane na yatima;
lakini huipotosha njia ya waovu.
10Mwenyezi-Mungu atawala milele,
Mungu wako, ee Siyoni, ni mfalme vizazi vyote!
Msifuni Mwenyezi-Mungu!

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 146: BHN

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha