Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 111

111
Mungu asifika kwa matendo yake
1Msifuni Mwenyezi-Mungu!
Nitamshukuru Mwenyezi-Mungu kwa moyo wangu wote,
nikijumuika na jamii ya watu waadilifu.
2Matendo ya Mwenyezi-Mungu ni makuu mno!
Wote wanaoyafurahia huyatafakari.
3Kila afanyacho kimejaa utukufu na fahari;
uadilifu wake wadumu milele.
4Amesababisha matendo yake ya ajabu yakumbukwe;
Mwenyezi-Mungu ni mwema na mwenye huruma.
5Huwapa chakula wenye kumcha;
hasahau kamwe agano lake.
6Amewaonesha watu wake nguvu ya matendo yake,
amewapa nchi za mataifa mengine ziwe mali yao.
7Matendo yake ni ya haki na ya kuaminika;
kanuni zake zote ni za kutegemewa.
8Amri zake zadumu daima na milele;
zimetolewa kwa haki na uadilifu.
9Aliwakomboa watu wake
na kufanya nao agano la milele.
Yeye ni mtakatifu na wa kutisha mno!
10Kumcha Mwenyezi-Mungu ni msingi wa hekima;
wote wanaozitii amri zake hujaliwa busara.
Sifa zake zadumu milele.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 111: BHN

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha