Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Methali 19:3-12

Methali 19:3-12 BHN

Mtu akijiangamiza kwa upumbavu wake, huielekeza hasira yake dhidi ya Mwenyezi-Mungu. Mali huvuta marafiki wengi wapya, lakini maskini huachwa bila rafiki. Shahidi mwongo hataacha kuadhibiwa; asemaye uongo hataepa adhabu. Watu wengi hujipendekeza kwa wakuu; kila mtu hutaka kuwa rafiki ya mtu mkarimu. Maskini huchukiwa na ndugu zake; marafiki zake ndio zaidi: Humkimbia! Hata awabembeleze namna gani hatawapata. Ajipatiaye hekima anaipenda nafsi yake; anayezingatia busara atastawi. Shahidi mwongo hatakosa kuadhibiwa; asemaye uongo ataangamia. Haifai kwa mpumbavu kuishi kwa anasa, tena ni vibaya zaidi mtumwa kuwatawala wakuu. Mwenye busara hakasiriki upesi; kusamehe makosa ni fahari kwake. Ghadhabu ya mfalme ni kama ngurumo ya simba, lakini wema wake ni kama umande juu ya majani.

Soma Methali 19