Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Yuda UTANGULIZI

UTANGULIZI
Barua hii ya Yuda imeandikwa sio kwa jumuiya fulani ya kanisa, bali kwa jumuiya yote ya Kikristo. Mwandishi anajitaja kama “Yuda, nduguye Yakobo”. Katika Injili ya Marko hao wawili, Yuda na Yakobo, wanasemekana kuwa “nduguze Yesu”. Tunajua mengi juu ya Yakobo, kwamba yeye alikuwa na nafasi muhimu ya uongozi wa jumuiya ya waumini wa Kanisa la Yerusalemu, na pia mwandishi wa barua inayotajwa kwa jina lake. Lakini hatujui mengine juu ya Yuda.
Mwandishi anatuambia kwamba alikuwa na lengo lake la kuandika juu ya msingi wa imani, lakini akalazimika kubadili na kuandika barua hii ya kuwashutumu waenezi wa mafundisho ya uongo ambao walijipenyeza kwa siri katika jumuiya ya waumini (3-16). Mwandishi anawaonya waumini wadumu imara katika imani (17-23) na kumalizia kwa utenzi wa sifa “kwake yeye aliye peke yake Mungu, Mkombozi wetu, uwe utukufu, ukuu, nguvu na mamlaka kwa njia ya Kristo Bwana wetu, tangu zama zote, sasa na hata milele! Amina” (24-25).

Iliyochaguliwa sasa

Yuda UTANGULIZI: BHN

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha