Yeremia 51:15-16
Yeremia 51:15-16 BHN
Mwenyezi-Mungu ndiye aliyeumba dunia kwa nguvu yake, aliyeuimarisha ulimwengu kwa hekima yake, na kwa maarifa yake akazitandaza mbingu. Anapotoa sauti yake maji hutitima mbinguni, hufanya ukungu upande kutoka mipaka ya dunia. Hufanya umeme umulike wakati wa mvua huvumisha upepo kutoka ghala zake.

