Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Hagai UTANGULIZI

UTANGULIZI
Tunavyoambiwa mwanzoni mwa kitabu hiki, Hagai alihubiri kuanzia mwaka wa pili wa utawala wa Dario mfalme wa Persia, yaani katika mwaka wa 520 K.K., karibu miaka 20 baada ya Wayahudi waliokuwa uhamishoni Babuloni kuruhusiwa na mfalme wa Persia kurudi makwao. Kundi la kwanza la Waisraeli lilirejea makwao kuanzia mwaka wa 538 K.K. Baada ya Wayahudi kurejea makwao, walianza shughuli za kujenga upya hekalu lililoharibiwa na Wababuloni katika mwaka wa 587. Lakini walikata tamaa; ndio maana nabii anawatia moyo waendelee. Anawatangazia kwamba, hekalu jipya litapendeza kuliko lile la kwanza (2:1-9) na kwamba ujenzi wake utamaliza hali ya unajisi na umaskini uliowapata watu wa Mungu (2:10-20).
Hagai aliwatia watu moyo kwa maneno yake, yaliyowahimiza watu wa nyakati zake wawe na bidii na kufanya kazi wakitazamia hali mpya ambayo Mungu amewatayarishia.

Iliyochaguliwa sasa

Hagai UTANGULIZI: BHN

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha