Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 1

1
KITABU CHA KWANZA
(Zaburi 1–41)
Furaha ya kweli
1Heri mtu asiyefuata shauri la waovu,
asiyeshiriki njia za wenye dhambi,
wala kujumuika na wenye dharau;
2bali huifurahia sheria ya Mwenyezi-Mungu,
na kuitafakari mchana na usiku.
3Huyo ni kama mti uliopandwa kando ya vijito,
unaozaa matunda kwa wakati wake,
na majani yake hayanyauki.
Kila afanyalo hufanikiwa.
4Lakini waovu sivyo walivyo;
wao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.
5Kwa hiyo watu waovu wataanguka wakati wa hukumu,
wenye dhambi hawatakaa na kusanyiko la waadilifu.
6Maana Mwenyezi-Mungu huziongoza njia za waadilifu;
lakini njia za waovu zitaishia katika maangamizi.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 1: BHND

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha