Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Mhubiri UTANGULIZI

UTANGULIZI
Kitabu cha Mhubiri (Kiebrania: “Kohelethi”, Kilatini: “Eklesiastes”) kina mawaidha ya mtu ambaye alitafakari sana juu ya ufupi wa maisha ya mwanadamu na mambo yake ya kutatiza, akachunguza na falsafa yake, akayaona hayo yote kuwa magumu yasiyoeleweka: “Kila kitu ni bure kabisa”. Katika huko kuwaza na kuwazua kwake anaona kwamba haiwezekani kuelewa mipango ya Mungu ambaye anaongoza mambo duniani. Hata hivyo anawahimiza watu wafanye kazi kwa bidii na kufurahia vipaji walivyopewa na Mungu muda wote waishipo.
Mwandishi: Hatuna mengi ya kuweza kumtambulisha ila ianaonekana kwamba alikuwa mmojawapo wa watu wenye hekima nyakati za utamaduni wa Kigiriki katika Mashariki ya kati ya Kale. Alikuwa mtu mwenye kufikiri sana na ambaye hakutosheka tu na kurudiarudia mawazo na mapokeo ya nyakati zake. Ingawa anamtaja mfalme Solomoni “mwana wa Daudi, mfalme huko Yerusalemu” (1:1,12) na pia anaposema juu ya kazi na utajiri wake (2:4-9), mambo anayoyazungumzia ni ya wakati wa baadaye sana.
Fikira nyingi za Mhubiri huyu zaonekana kuwa za kutatiza na za mashaka. Hata hivyo anao msimamo wa kidini na anatushauri mwishoni: “Mche Mungu, na uzishike amri zake; kwa sababu hilo ndilo jukumu aliloumbiwa mwanadamu” (12:13).

Iliyochaguliwa sasa

Mhubiri UTANGULIZI: BHND

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha