Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

1 Timotheo UTANGULIZI

UTANGULIZI
Timotheo alikuwa mwana wa mama mmoja Myahudi na baba yake alikuwa Mgiriki. Katika kitabu cha Matendo ya Mitume na katika barua nyingine za Paulo, tunajua kwamba Timotheo aliandamana na Paulo katika ziara zake na kumsaidia katika kazi yake ya kuhubiri Habari Njema (taz Mate 17:14-15; 18:5; 19:22 na 1Kor 4:17; 16:10-11; Fil 2:19-24; n.k.). Barua hii ya kwanza na ile ya pili pamoja na barua kwa Tito zaitwa pia barua za “kichungaji” kwa vile zinawapa mwongozo hao “wachungaji” au viongozi wa Kanisa.
Barua hii ya kwanza kwa Timotheo yahusu mambo matatu makubwa:
Kwanza Paulo anaonya jumuiya ya Wakristo ijihadhari na mafundisho ya uongo yaliyochanganya fikira za Kiyahudi na za watu wasio Wayahudi, mafundisho ambayo yalikuwa yanaendelezwa na baadhi ya watu. Baadhi ya mafundisho hayo yaliwaaminisha watu kwamba ulimwengu huu unaoonekana ni mbaya na kwamba mtu anaweza tu kuokoka kwa kujua siri fulani ambazo wamepewa tu watu fulani. Zaidi ya hayo watu walitakiwa kufuata mazoezi yaliyohusika na kuacha kula vyakula fulanifulani. Kisha Paulo anatoa mwongozo kuhusu ibada, muundo na mpango katika jumuiya ya Wakristo au Kanisa na tabia ya viongozi wake.
Mwisho anatoa mashauri yake kwa Timotheo kuhusu namna ya kutekeleza utumishi wake na kujishughulisha na makundi mbalimbali ya waumini ili apate kuwa kweli “mtumishi mwema wa Kristo Yesu” (4:6).

Iliyochaguliwa sasa

1 Timotheo UTANGULIZI: BHND

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha