Mateo 1:18-19
Mateo 1:18-19 SRB37
Kuzaliwa kwake Yesu Kristo kulikuwa hivi: Maria, mama yake, alionekana ana mimba kwa nguvu ya Roho Mtakatifu hapo, alipokuwa ameposwa na Yosefu, nao walikuwa hawajakaribiana. Yosefu, mchumba wake, alikuwa mwongofu, tena hakutaka kumwumbua, kwa hiyo alitaka kumwacha tu, watu wasijue.