Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Mwanzo Utangulizi

Utangulizi
Kitabu hiki kiliandikwa kuelezea vile vitu vyote vilianza. Neno “Mwanzo” linatokana na maana ya “asili” au “chanzo.” Kinaelezea kwamba Mwenyezi Mungu aliumba ulimwengu wote, vile mwanadamu aliumbwa na kuwekwa katika mazingira yaliyokuwa kamili, vile dhambi ilianza, na vile Mwenyezi Mungu alitoa wokovu kwa mwanadamu aliyepotea. Mwanzo wa historia ya mwanadamu unaelezewa, mwanzo wa sanaa na mwanadamu kutengeneza vifaa, vile lugha za wanadamu zilianza, na kule mataifa tofauti yalitokea. Kitabu kinaendelea kuelezea chanzo cha Waebrania naye Ibrahimu, akifuatiwa na habari za Isaka, Yakobo na wanawe, na kitabu kinaishia na Yusufu akiwa Misri.
Wazo Kuu
Wazo kuu katika kitabu hiki ni kwamba, ingawa Mwenyezi Mungu aliumba vitu vyote vikiwa vizuri nayo dhambi ya mwanadamu ikaviharibu, Mwenyezi Mungu hajakufa moyo, bali sasa anamtafuta mwanadamu ili kumwokoa. Mamlaka ya Mwenyezi Mungu juu ya mambo yote yanasisitizwa, mtazamo wa kipekee ukiwa vile Mwenyezi Mungu anaendesha historia kuleta wema kwa watu wake na wokovu wao (50:20).
Mwandishi
Musa.
Tarehe
Kama mwaka wa 1420 au 1220 KK.
Mgawanyo
Kuumbwa kwa ulimwengu, na mwanadamu (1:1–2:25)
Kuanguka kwa mwanadamu, na chanzo cha dhambi (3:1–4:26)
Historia ya mwanadamu aliyeanguka hadi gharika (5:1–9:29)
Binadamu kuenea duniani kote (10:1–11:32)
Maisha ya Ibrahimu (12:1–25:18)
Maisha ya Isaka (25:19–26:35)
Maisha ya Yakobo na Esau (27:1–37:1)
Maisha ya Yusufu (37:2–50:26).

Iliyochaguliwa sasa

Mwanzo Utangulizi: NMM

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha