Zaburi 134
134
Msifuni Mungu#134 Zaburi hii ni ya mwisho ya fungu la zaburi zenye anwani “Wimbo wa Kwenda Juu” (taz Zab 120).
(Wimbo wa Kwenda Juu)
1Njoni kumsifu Mwenyezi-Mungu enyi watumishi wake wote,
enyi nyote mnaotumikia usiku nyumbani mwake.
2Inueni mikono kuelekea mahali patakatifu,
na kumtukuza Mwenyezi-Mungu!
3Mwenyezi-Mungu awabariki kutoka Siyoni;#134:3 Mwenyezi-Mungu awabariki kutoka Siyoni: Maneno haya huenda yalitamkwa na kuhani kuwatakia baraka mahujaji waliofika Yerusalemu kwa sikukuu fulani. Taz pia 104.
yeye aliyeumba mbingu na dunia.
Iliyochaguliwa sasa
Zaburi 134: BHNTLK
Kuonyesha
Shirikisha
Nakili

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia
Copyright The Bible Society of Tanzania, 1993
The Bible Society of Kenya 1993