Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 92

92
Shukrani kwa ajili ya uthibitisho
Zaburi. Wimbo wa siku ya Sabato.
1Ni neno jema kumshukuru BWANA,
Na kuliimbia jina lako sifa, Ee Uliye Juu.
2Kuzitangaza rehema zako asubuhi,
Na uaminifu wako wakati wa usiku.
3Kwa chombo chenye nyuzi kumi,
Na kwa kinanda,
Na kwa mlio wa kinubi.
4Kwa kuwa umenifurahisha, BWANA,
Kwa kazi yako; nitashangilia
Kwa ajili ya matendo ya mikono yako.
5 # Isa 28:29; Rum 11:23 Ee BWANA, jinsi yalivyo makuu matendo yako!
Mawazo yako ni mafumbo makubwa.
6 # Zab 73:22 Mtu mjinga hayatambui hayo,
Wala mpumbavu hayafahamu.
7 # Ayu 21:7; Yer 12:1; Mal 3:15 Hata wasio haki wakichipuka kama majani
Na wote watendao maovu wakastawi.
Mwishowe wataangamizwa milele;
8Bali Wewe, BWANA, U Mtukufu hata milele.
9Maana hao adui zako, Ee BWANA,
Hao adui zako watapotea,
Na watendao maovu watatawanyika wote pia.
10Bali pembe yangu umeiinua kama pembe ya nyati,
Nimepakwa mafuta mabichi.
11Na jicho langu limeona kuanguka kwa adui zangu,
Sikio langu limesikia maangamizi ya waovu walionishambulia.
12 # Zab 52:8; Wim 7:7 Mwenye haki atastawi kama mtende,
Atakua kama mwerezi wa Lebanoni.
13 # Isa 60:21; Mt 15:13; Yn 15:2,5 Waliopandwa katika nyumba ya BWANA
Watastawi katika nyua za Mungu wetu.
14Watazaa matunda hadi wakati wa uzee,
Watajaa utomvu, watakuwa na ubichi.
15 # Kum 32:4; Rum 9:14 Watangaze ya kuwa BWANA ni mwenye adili,
Mwamba wangu, ndani yake hamna udhalimu.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 92: SRUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha