Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 81:1-16

Zaburi 81:1-16 SRUV

Mwimbieni Mungu, nguvu zetu, nyimbo za furaha, Mshangilieni Mungu wa Yakobo. Pazeni zaburi, pigeni matari, Kinubi chenye sauti nzuri, na kinanda. Pigeni panda mwandamo wa mwezi, Kukiwa na mbalamwezi, wakati wa sikukuu yetu. Kwa maana ni sheria kwa Israeli, Ni hukumu ya Mungu wa Yakobo. Aliamuru iwe ushuhuda katika Yusufu, Alipoondoka juu ya nchi ya Misri; Maneno yake nisiyemjua niliyasikia. Nimeutua mzigo begani mwake; Mikono yake nikaiondolea kazi nzito. Katika shida uliniita nikakuokoa; Nilikuitikia kutoka maficho yangu ya radi; Nilikujaribu penye maji ya Meriba. Enyi watu wangu, sikieni, nami nitawaonya, Ee Israeli, kama ukitaka kunisikiliza; Usiwe na mungu mgeni ndani yako; Wala usimsujudie mungu mwingine. Mimi ndimi BWANA, Mungu wako, Niliyekupandisha toka nchi ya Misri; Fumbua sana kinywa chako nami nitakijaza. Lakini watu wangu hawakuisikiliza sauti yangu, Wala Israeli hawakunitaka. Nikawaacha wakaenda kwa ukaidi wa mioyo yao, Waenende katika mashauri yao. Laiti watu wangu wangenisikiliza, Na Israeli angeenenda katika njia zangu; Ningewadhili adui zao kwa upesi, Na juu ya watesi wao ningegeuza mkono wangu; Wamchukiao BWANA wangenyenyekea mbele zake, Na maangamizi yao yangedumu milele. Naam, ningewalisha kwa ngano iliyo bora zaidi, Ningewashibisha kwa asali itokayo mwambani.

Soma Zaburi 81

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha