Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 24

24
Kuingia hekaluni
Ya Daudi. Zaburi.
1 # 1 Kor 10:26; Kut 9:29; Ayu 41:11 Nchi na vyote vilivyomo ni mali ya BWANA,
Dunia na wote wakaao ndani yake.
2Maana ameiweka misingi yake juu ya bahari,
Na juu ya mito ya maji aliithibitisha.
3Ni nani atakayepanda katika mlima wa BWANA?
Ni nani atakayesimama katika patakatifu pake?
4 # Mt 5:8 Mtu aliye na mikono safi na moyo mweupe,
Asiyeiweka nafsi yake katika uongo,
Wala hakuapa kwa hila.
5Atapokea baraka kwa BWANA,
Na haki kwa Mungu wa wokovu wake.
6Hiki ndicho kizazi cha wamtafutao,
Wakutafutao uso wako, Ee Mungu wa Yakobo.
7 # Hag 2:7; Mal 3:1; 1 Kor 2:8 Inueni vichwa vyenu, enyi malango,
Inukeni, enyi malango ya milele,
Mfalme wa utukufu apate kuingia.
8Ni nani Mfalme wa utukufu?
BWANA mwenye nguvu, hodari,
BWANA hodari wa vita.
9Inueni vichwa vyenu, enyi malango,
Naam, viinueni, enyi malango ya milele,
Mfalme wa utukufu apate kuingia.
10Ni nani huyu Mfalme wa utukufu?
BWANA wa majeshi,
Yeye ndiye Mfalme wa utukufu.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 24: SRUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha