Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 148:1-14

Zaburi 148:1-14 SRUV

Haleluya. Msifuni BWANA kutoka mbinguni; Msifuni katika mahali palipo juu. Msifuni, enyi malaika wake wote; Msifuni, majeshi yake yote. Msifuni, jua na mwezi; Msifuni, nyota zote zenye mwanga. Msifuni, enyi mbingu za mbingu, Nanyi maji mlioko juu ya mbingu. Na vilisifu jina la BWANA, Kwa maana aliamuru, vikaumbwa. Amevithibitisha hata milele na milele, Ametoa amri wala haitapita. Msifuni BWANA kutoka nchi, Enyi nyangumi na vilindi vyote. Moto na mvua ya mawe, theluji na mvuke, Upepo wa dhoruba utimizao neno lake. Milima na vilima vyote, Miti yenye matunda na mierezi yote. Hayawani, na wanyama wafugwao, Vitambaavyo, na ndege wenye mbawa. Wafalme wa dunia, na watu wote, Wakuu, na watawala wote wa dunia. Vijana wa kiume, na wanawali, Wazee, na watoto; Na walisifu jina la BWANA, Maana jina lake peke yake limetukuka; Adhama yake i juu ya nchi na mbingu. Naye amewainulia watu wake pembe, Sifa za watauwa wake wote; Wana wa Israeli, watu walio karibu naye. Haleluya.

Soma Zaburi 148

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Zaburi 148:1-14

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha