Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 119:121-128

Zaburi 119:121-128 SRUV

Nimefanya hukumu na haki, Usiniache mikononi mwao wanaonionea. Uwe mdhamini wa mtumishi wako, apate mema, Wenye kiburi wasinionee. Macho yangu yanafifia kwa kuungojea wokovu wako, Na kutimizwa kwa ahadi yako ya haki. Kama zilivyo rehema zako umtendee mtumishi wako, Na amri zako unifundishe. Mimi ni mtumishi wako, unifahamishe, Nipate kuzijua shuhuda zako. Wakati umewadia BWANA atende kazi; Kwa kuwa wameitangua sheria yako. Ndiyo maana nimeyapenda maagizo yako, Kuliko dhahabu, naam, dhahabu iliyo safi. Maana nayafuata mausia yako yote, kuwa ya adili, Kila njia ya uongo naichukia.

Soma Zaburi 119

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha