Zaburi 101:1-3
Zaburi 101:1-3 SRUV
Rehema na hukumu nitaziimba, Ee BWANA, nitakuimbia zaburi. Nitakuwa na mwenendo usio na hatia; Utakuja kwangu lini? Nitakwenda kwa unyofu wa moyo Ndani ya nyumba yangu. Sitaweka mbele ya macho yangu Neno la uovu. Kazi yao waliopotoka naichukia, Haitaambatana nami.