Mithali 26:13-16
Mithali 26:13-16 SRUV
Mtu mvivu husema, Simba yuko njiani, Simba yuko katika njia kuu. Kama vile mlango ugeukavyo katika bawaba zake; Kadhalika mtu mvivu katika kitanda chake. Mtu mvivu hutia mkono wake katika sahani; Kwamchosha kuupeleka tena kinywani pake. Mtu mvivu ni mwenye hekima machoni pake, Kuliko watu saba wawezao kutoa sababu.