Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Mathayo 21:14-17

Mathayo 21:14-17 SRUV

Na vipofu na viwete wakamwendea mle hekaluni, akawaponya. Lakini wakuu wa makuhani na waandishi walipoyaona maajabu aliyoyafanya, na watoto waliopaza sauti zao hekaluni, wakisema, Hosana, Mwana wa Daudi! Walikasirika, wakamwambia, Wasikia hawa wasemavyo? Yesu akawaambia, Naam; hamkupata kusoma, Kwa vinywa vya watoto wachanga na wanyonyao umejiandalia sifa? Akawaacha, akatoka nje ya mji mpaka Bethania, akalala huko.

Soma Mathayo 21