Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Ayubu 36

36
Elihu asifia wema wa Mungu
1Tena Elihu akaendelea na kusema,
2Ningojee kidogo nami nitakueleza;
Kwa kuwa ningali na maneno kwa ajili ya Mungu.
3Nitayaleta maarifa yangu kutoka mbali,
Nami nitampa haki Muumba wangu.
4Maana hakika maneno yangu si ya uongo;
Aliyekamilika katika maarifa yu pamoja nawe.
5Tazama, Mungu ni hodari, wala hamdharau mtu yeyote;
Ana uweza katika nguvu za fahamu.
6Hauhifadhi uhai wa waovu;
Lakini huwapa wateswao haki yao.
7 # Zab 113:8 Yeye hawaondolei macho yake wenye haki;
Lakini pamoja na wafalme huwaweka
Katika viti vya enzi milele, nao hutukuzwa.
8 # Zab 107:10 Nao wakifungwa kwa pingu,
Wakitwaliwa kwa kamba za mateso;
9Ndipo huwaonesha matendo yao,
Na makosa yao, ya kuwa wametenda kwa kujivuna.
10Yeye huyafunua masikio yao, wasikie maonyo,
Na kuwaagiza warudi kuuacha uovu.
11 # Ayu 11:13-19; Isa 1:19; 1 Tim 4:8; Yak 5:5 Kama wakisikia na kumtumikia,
Watapisha siku zao katika kufanikiwa,
Na miaka yao katika furaha.
12Lakini wasiposikia, wataangamia kwa upanga,
Nao watakufa pasipo maarifa.
13Lakini hao wasiomcha Mungu mioyoni hujiwekea hasira
Hawalilii msaada hapo awafungapo.
14Wao hufa wakingali vijana,
Na uhai wao huangamia katikati ya wachafu.
15Yeye humponya aliyetaabika kwa njia ya taabu yake,
Na kuyafunua masikio yao kwa maonevu.
16Naam, yeye angekuongoza utoke katika msiba
Hata mahali penye nafasi, ambapo hapana kizuizi;
Na kilichowekwa mezani pako kingejaa mafuta.
17Lakini umejaa hukumu ya waovu;
Hukumu na haki hukushika.
18Basi ujitunze, isije hasira ikakuvuta hata ukafanya mzaha;
Wala usikubali ukuu wa ukombozi ukugeuze.
19Je! Mali yako itatosha, hata usiwe katika taabu,
Au uwezo wote wa nguvu zako?
20Usiutamani usiku,
Wakati watu wakatwapo katika mahali pao.
21 # Ebr 11:25 Jitunze, usiutazame uovu;
Kwani umeuchagua huo zaidi ya taabu.
22 # Isa 40:13; Rum 11:34; 1 Kor 2:16 Tazama, Mungu hutenda makuu kwa uweza wake;
Ni nani afundishaye kama yeye?
23 # Kum 32:4 Ni nani aliyemwagiza njia yake?
Au ni nani awezaye kusema, Wewe umetenda yasiyo haki?
Elihu atangaza ukuu wa Mungu
24 # Zab 33:4; Dan 4:37; Yer 9:24; 1 Kor 1:31; 2 Kor 10:17; Ufu 15:3 Kumbuka kuitukuza kazi yake,
Watu waliyoiimbia.
25 # Rum 1:19 Wanadamu wote wameitazama;
Watu huiangalia kwa mbali.
26 # 1 Kor 13:12; Zab 90:2; Ebr 1:12 Tazama, Mungu ni mkuu, nasi hatumjui;
Hesabu ya miaka yake haichunguziki.
27Maana yeye huvuta juu matone ya maji,
Yamwagikayo katika mvua kutoka ukungu wake;
28Ambayo mawingu yainyesha
Na kudondoza juu ya wanadamu kwa wingi.
29Naam, mtu aweza kuelewa matandazo ya mawingu,
Ngurumo za makao yake?
30Tazama, yeye huutandaza mwanga wake, umzunguke;
Naye hufunika vilindi vya bahari.
31Kwani huwahukumu makabila ya watu kwa njia hizi;
Hutoa chakula kwa ukarimu.
32Yeye huifunika mikono yake kwa umeme;
Na kuuagiza shabaha utakayopiga.
33Mshindo wake hutoa habari zake,
Anayewaka hasira juu ya uovu.

Iliyochaguliwa sasa

Ayubu 36: SRUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha