Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

1 Petro 3

3
Wake na waume
1 # Efe 5:22; Kol 3:18; Tit 2:5 Kadhalika ninyi wake, watiini waume zenu; kusudi, ikiwa wako wasioliamini Neno, wavutwe kwa mwenendo wa wake zao, pasipo lile Neno; 2#1 Pet 2:12 wakiutazama mwenendo wenu safi, na wa hofu. 3#1 Tim 2:9; Isa 3:18-24 Kujipamba kwenu, kusiwe kujipamba kwa nje, yaani, kusuka nywele; na kujitia dhahabu, na kuvalia mavazi; 4bali kuwe utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; yaani, roho ya upole na utulivu, iliyo ya thamani kuu mbele za Mungu. 5Maana hivyo ndivyo walivyojipamba wanawake watakatifu wa zamani, waliomtumaini Mungu, na kuwatii waume zao. 6#Mwa 18:12; Mit 3:25 Kama vile Sara alivyomtii Abrahamu, akamwita bwana; nanyi ni watoto wake, mfanyapo mema, pasipo kutishwa na hofu yoyote. 7#Efe 5:25; Kol 3:19 Kadhalika ninyi waume, kaeni na wake zenu kwa akili; na kumpa mke heshima, kama chombo kisicho na nguvu; maana wao pia ni warithi wa neema ya uzima, ili maombi yenu yasizuiliwe na chochote.
Mateso kwa ajili ya kutenda Haki
8 # Rum 12:16 Neno la mwisho ni hili; muwe na nia moja, wenye kuhurumiana, wenye kupendana kama ndugu, wasikitikivu, wanyenyekevu; 9#Zab 34:12-16; Yak 1:26; Mt 5:44; 1 The 5:15; 1 Pet 2:23 watu wasiolipa baya kwa baya, au laumu kwa laumu; bali wenye kubariki; kwa sababu hayo ndiyo mliyoitiwa ili mrithi baraka. 10#Zab 34:12-16; Yak 1:26 Kwa maana,
Atakaye kupenda maisha,
Na kuona siku njema,
Auzuie ulimi wake usinene mabaya,
Na midomo yake isiseme uongo.
11Na aache mabaya, atende mema;
Atafute amani, aifuate sana.
12Kwa kuwa macho ya Bwana huwaelekea wenye haki,
Na masikio yake husikiliza maombi yao;
Bali uso wa Bwana uko juu ya watenda mabaya.
13Naye ni nani atakayewadhuru, mkiwa wenye juhudi katika mema? 14#Mt 5:10; Isa 8:12-13; 1 Pet 2:20 Lakini hata mkiteswa kwa sababu ya kutenda haki, mna heri. Msiogope kutisha kwao, wala msifadhaike; bali mtakaseni Kristo Bwana mioyoni mwenu. 15#Isa 8:13; Kol 4:6; 1 Pet 1:3,13 Muwe tayari siku zote kumjibu kila mtu awaulizaye habari za tumaini lililo ndani yenu; lakini kwa upole na kwa heshima. 16#1 Pet 2:12 Nanyi muwe na dhamiri njema, ili katika neno lile mnalosingiziwa, watahayarishwe wale wautukanao mwenendo wenu mwema katika Kristo. 17#1 Pet 2:20-24 Maana ni afadhali kuteswa kwa kutenda mema, ikiwa ndiyo mapenzi ya Mungu, kuliko kwa kutenda mabaya. 18#Rum 6:10; Efe 2:18; Ebr 9:28; 10:10 Kwa maana Kristo naye aliteswa mara moja kwa ajili ya dhambi, mwenye haki kwa ajili yao wasio haki, ili atulete kwa Mungu; akauawa kimwili, lakini akahuishwa kiroho, 19#1 Pet 4:8 ambayo kwa hiyo aliwaendea roho waliokaa kifungoni, akawahubiria; 20#Mwa 6:1—7:7,17,24 watu wasiotii hapo zamani, wakati Mungu alipowavumilia kwa subira, siku za Nuhu, safina ilipokuwa ikitengenezwa; ambamo ndani yake wachache, yaani, watu wanane, waliokoka kwa maji. 21#Efe 5:26; Ebr 10:22 Mfano wa mambo hayo ni ubatizo, unaowaokoa ninyi pia siku hizi; (siyo kuwekea mbali uchafu wa mwili, bali jibu la dhamiri safi mbele za Mungu), kwa kufufuka kwake Yesu Kristo. 22#Efe 1:20,21; Zab 110:1; Kol 1:16 Naye yuko katika mkono wa kulia wa Mungu, amekwenda zake mbinguni, malaika na enzi na nguvu zikiisha kutiishwa chini yake.

Iliyochaguliwa sasa

1 Petro 3: SRUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha