Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

1 Wakorintho 13

13
Karama ya upendo
1Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao. 2#Mt 17:20; 7:22; 21:21; Mk 11:23 Tena nijapokuwa na unabii, na kujua siri zote na maarifa yote, nijapokuwa na imani timilifu kiasi cha kuweza kuhamisha milima, kama sina upendo, mimi si kitu. 3#Mt 6:2 Tena nikitoa mali zangu zote kuwalisha maskini, tena nikijitoa mwili wangu niungue moto, kama sina upendo, hainifaidi kitu. 4Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni; 5#Zek 8:17; Flp 2:4 haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya; 6#Rum 12:9 haufurahii udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli; 7#Mit 10:12; 1 Kor 9:12; Rum 15:1 huvumilia yote; huamini yote; hutumaini yote; hustahimili yote. 8#1 Pet 4:8 Upendo haupungui neno wakati wowote; bali ukiwapo unabii utabatilika; zikiwapo lugha, zitakoma; yakiwapo maarifa, yatabatilika. 9Kwa maana tunafahamu kwa sehemu; na tunafanya unabii kwa sehemu; 10lakini ijapo ile iliyo kamili, iliyo kwa sehemu itabatilika. 11Nilipokuwa mtoto mchanga, nilisema kama mtoto mchanga, nilifahamu kama mtoto mchanga, nilifikiri kama mtoto mchanga; tokea hapo nilipokuwa mtu mzima, nimeyabatilisha mambo ya kitoto. 12#2 Kor 5:7; Yak 1:23 Maana sasa tunaona kwa kioo kwa jinsi ya fumbo; wakati ule tutaona uso kwa uso; sasa nafahamu kwa sehemu; wakati ule nitajua sana kama mimi nami ninavyojuliwa sana. 13#1 The 1:3; 1 Yoh 4:16 Basi, sasa inadumu imani, tumaini, upendo, haya matatu; na katika hayo lililo kuu ni upendo.

Iliyochaguliwa sasa

1 Wakorintho 13: SRUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha