Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zab 14

14
Kushutumiwa kwa Wasiomwamini Mungu
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.
1 # Rum 3:10-12; Zab 10:4; Mit 1:7,22; Mwa 6:12 Mpumbavu amesema moyoni, Hakuna Mungu;
Wameharibu matendo yao na kuyafanya chukizo,
Hakuna atendaye mema.
2Toka mbinguni BWANA aliwachungulia wanadamu,
Aone kama yuko mtu mwenye akili,
Amtafutaye Mungu.
3Wote wamepotoka, wameoza wote pamoja,
Hakuna atendaye mema,
La! Hata mmoja.
4Je! Wote wafanyao maovu hawajui?
Walao watu wangu kama walavyo mkate,
Hawamwiti BWANA.
5Hapo ndipo walipoingiwa na hofu nyingi,
Maana Mungu yupo pamoja na kizazi cha haki.
6Mnalitia aibu shauri la mtu mnyonge,
Bali BWANA ndiye aliye kimbilio lake.
7Laiti wokovu wa Israeli utoke katika Sayuni!
BWANA awarudishapo wafungwa wa watu wake;
Yakobo atashangilia,
Israeli atafurahi.

Iliyochaguliwa sasa

Zab 14: SUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha