Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zab 119:153-160

Zab 119:153-160 SUV

Uyaangalie mateso yangu, uniokoe, Maana sikuisahau sheria yako. Unitetee na kunikomboa, Unihuishe sawasawa na ahadi yako. Wokovu u mbali na wasio haki, Kwa maana hawajifunzi amri zako. Ee BWANA, rehema zako ni nyingi, Unihuishe sawasawa na hukumu zako. Wanaonifuatia na watesi wangu ni wengi, Lakini sikujiepusha na shuhuda zako. Nimewaona watendao uhaini nikachukizwa, Kwa sababu hawakulitii neno lako. Uangalie niyapendavyo mausia yako, Ee BWANA, unihuishe sawasawa na fadhili zako. Jumla ya neno lako ni kweli, Na kila hukumu ya haki yako ni ya milele.

Soma Zab 119

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha