Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zab 119:121-128

Zab 119:121-128 SUV

Nimefanya hukumu na haki, Usiniache mikononi mwao wanaonionea. Uwe mdhamini wa mtumishi wako, apate mema, Wenye kiburi wasinionee. Macho yangu yamefifia kwa kuutamani wokovu wako, Na ahadi ya haki yako. Kama zilivyo rehema zako umtendee mtumishi wako, Na amri zako unifundishe. Mimi ni mtumishi wako, unifahamishe, Nipate kuzijua shuhuda zako. Wakati umewadia BWANA atende kazi; Kwa kuwa wameitangua sheria yako. Ndiyo maana nimeyapenda maagizo yako, Kuliko dhahabu, naam, dhahabu iliyo safi. Maana nayaona mausia yako yote kuwa ya adili, Kila njia ya uongo naichukia.

Soma Zab 119

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha