Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zab 114

114
Maajabu ya Mungu Wakati wa kutoka Misri
1 # Kut 12:51 Haleluya.
Israeli alipotoka Misri,
Na Yakobo katika watu wa lugha ya kigeni.
2Yuda ilikuwa patakatifu pake,
Israeli milki yake.
3 # Kut 14:21; Yos 3:16 Bahari iliona ikakimbia,
Yordani ilirudishwa nyuma.
4 # Zab 29:6; 68:16; Hab 3:6 Milima iliruka kama kondoo waume,
Vilima kama wana-kondoo.
5Ee bahari, una nini, ukimbie?
Yordani, urudi nyuma?
6Enyi milima, mruke kama kondoo waume?
Enyi vilima, kama wana-kondoo?
7Tetemeka, Ee nchi, mbele za uso wa Bwana,
Mbele za uso wa Mungu wa Yakobo.
8 # Kut 17:1-7; Hes 20:2-13; Zab 107:35 Augeuza mwamba kuwa ziwa la maji,
Jiwe gumu kuwa chemchemi.

Iliyochaguliwa sasa

Zab 114: SUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha