Usiseme masikioni mwa mpumbavu; Maana atadharau hekima ya maneno yako. Usiiondoe alama ya mpaka wa zamani; Wala usiingie katika mashamba ya yatima; Kwa sababu mkombozi wao ana nguvu; Atawatetea juu yako. Elekeza moyo wako kusikiliza mafundisho; Tega masikio yako kusikia maneno ya maarifa. Usimnyime mtoto wako mapigo; Maana ukimpiga kwa fimbo hatakufa. Utampiga kwa fimbo, Na kumwokoa nafsi yake na Kuzimu. Mwanangu, kama moyo wako una hekima, Moyo wangu utafurahi, naam, moyo wangu; Naam, viuno vyangu vitafurahi, Midomo yako inenapo maneno mema. Moyo wako usiwahusudu wenye dhambi; Bali mche BWANA mchana kutwa; Maana bila shaka iko thawabu; Na tumaini lako halitabatilika.
Soma Mit 23
Shirikisha
Linganisha Matoleo Yote: Mit 23:9-18
Hifadhi mistari, soma bila mtandao, tazama klipu za mafunzo, na zaidi!
YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha
Nyumbani
Biblia
Mipango
Video