Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Isa 53

53
1 # 1 Kor 1:18; Yn 12:38; Rum 10:16 Ni nani aliyesadiki habari tuliyoileta?
Na mkono wa BWANA amefunuliwa nani?
2 # Mk 9:12 Maana alikua mbele zake kama mche mwororo,
Na kama mzizi katika nchi kavu;
Yeye hana umbo wala uzuri;
Na tumwonapo hana uzuri hata tumtamani.
3 # Zab 22:6; Ebr 4:15; Yn 1:10 Alidharauliwa na kukataliwa na watu;
Mtu wa huzuni nyingi, ajuaye sikitiko;
Na kama mtu ambaye watu humficha nyuso zao,
Alidharauliwa wala hatukumhesabu kuwa kitu.
4 # Mt 8:17; 26:66; 1 Pet 2:24 Hakika ameyachukua masikitiko yetu,
Amejitwika huzuni zetu;
Lakini tulimdhania ya kuwa amepigwa,
Amepigwa na Mungu, na kuteswa.
5 # 1 Pet 2:24 Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu,
Alichubuliwa kwa maovu yetu;
Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake,
Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona.
6 # 1 Pet 2:25 Sisi sote kama kondoo tumepotea;
Kila mmoja wetu amegeukia njia yake mwenyewe;
Na BWANA ameweka juu yake
Maovu yetu sisi sote.
7 # Mdo 8:32; 1 Pet 1:19; Ufu 5:6 Alionewa, lakini alinyenyekea,
Wala hakufunua kinywa chake;
Kama mwana-kondoo apelekwaye machinjoni,
Na kama vile kondoo anyamazavyo
Mbele yao wakatao manyoya yake;
Naam, hakufunua kinywa chake.
8 # Dan 9:26 Kwa kuonewa na kuhukumiwa aliondolewa;
Na maisha yake ni nani atakayeisimulia?
Maana amekatiliwa mbali na nchi ya walio hai;
Alipigwa kwa sababu ya makosa ya watu wangu.
9 # Mt 27:57; 1 Pet 2:22 Wakamfanyia kaburi pamoja na wabaya;
Na pamoja na matajiri katika kufa kwake;
Ingawa hakutenda jeuri,
Wala hapakuwa na hila kinywani mwake.
10 # 2 Kor 5:21; Gal 3:13; Rum 6:9; Efe 1:5 Lakini BWANA aliridhika kumchubua;
Amemhuzunisha;
Utakapofanya nafsi yake kuwa dhabihu kwa dhambi,
Ataona uzao wake, ataishi siku nyingi,
Na mapenzi ya BWANA yatafanikiwa mkononi mwake;
11 # Yn 17:3; 1 Yoh 2:1; Rum 5:18 Ataona mazao ya taabu ya nafsi yake, na kuridhika.
Kwa maarifa yake mtumishi wangu mwenye haki
Atawafanya wengi kuwa wenye haki;
Naye atayachukua maovu yao.
12 # Flp 2:9; Kol 2:15; Mk 15:28; Lk 22:37; 23:34 Kwa hiyo nitamgawia sehemu pamoja na wakuu,
Naye atagawanya nyara pamoja nao walio hodari;
Kwa sababu alimwaga nafsi yake hata kufa,
Akahesabiwa pamoja na hao wakosao.
Walakini alichukua dhambi za watu wengi,
Na kuwaombea wakosaji.

Iliyochaguliwa sasa

Isa 53: SUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha