Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Isa 21

21
Utabiri juu ya Babeli, Edomu na Arabuni
1 # Zek 9:14 Ufunuo juu ya bara ya bahari. Kama tufani za Negebu#21:1Negebu tafsiri yake ni Nchi za kusini. zikaribiavyo kwa kasi, inakuja kutoka bara, toka nchi itishayo. 2#1 Sam 24:13; Yer 49:34; Isa 24:16; 13:17Nimeonyeshwa maono magumu; atendaye hila anatenda hila, mharibu anaharibu. Panda juu, Ee Elamu; husuru, Ee Umedi; mimi ninakomesha maombolezo yake yote. 3Kwa sababu hiyo viuno vyangu vimejaa maumivu, utungu umenishika, kama utungu wa mwanamke azaaye; ninaumwa sana, nisiweze kusikia; nimefadhaishwa wa hofu, nisiweze kuona. 4#Kum 28:67Moyo wangu unapiga-piga, utisho umenitaabisha, gizagiza la jioni nilipendalo limegeuka likanitetemesha. 5#Dan 5:5Wanaandika meza, wanaweka ulinzi, wanakula, wanakunywa. Simameni, enyi wakuu, itieni ngao mafuta. 6Maana Bwana ameniambia hivi, Enenda, weka mlinzi; aonayo na ayatangaze. 7Naye akiona kundi la wapanda farasi, wakienda wawili wawili, na kundi la punda, na kundi la ngamia; asikilize sana, akijitahidi kusikiliza. 8#Hab 2:1Ndipo akalia kama simba, Ee Bwana, mimi nasimama daima juu ya mnara wakati wa mchana, na kila usiku ninakaa katika zamu ya ulinzi wangu. 9#Isa 13:19; Yer 50:2; Ufu 14:8; 18:2Na, tazama, linakuja kundi la watu, wapanda farasi, wakienda wawili wawili. Akajibu na kusema, Babeli umeanguka, umeanguka; na sanamu zote za miungu yake zimevunjwa chini. 10#Yer 51:33; Mik 4:13; Hab 3:12Ewe niliyekufikicha, na nafaka ya sakafu yangu; Hayo niliyoyasikia kwa BWANA wa majeshi, Mungu wa Israeli, nimewapasha habari zake.
11 # 1 Nya 1:30; Eze 35:2; Oba 1:1 Ufunuo juu ya Duma. Mtu ananililia toka Seiri, Ee mlinzi, habari gani za usiku? Ee mlinzi, habari gani za usiku? 12Mlinzi akasema, Mchana unakuja na usiku pia; mkitaka kuuliza, ulizeni; njoni tena.
13 # 1 Nya 1:9 Ufunuo juu ya Arabuni.
Ndani ya msitu wa Arabuni mtalala,
Enyi misafara ya Wadedani.
14 # Ayu 6:19 Waleteeni wenye kiu maji,
Enyi wenyeji wa nchi ya Tema;
Nendeni kuwalaki wakimbiao na chakula chao.
15Kwa maana wanakimbia mbele ya panga,
Upanga uliofutwa, na upinde uliopindwa,
Na mbele ya ukali wa vita.
16 # Mwa 25:13; Zab 120:5; Wim 1:5; Isa 60:7 Kwa sababu Bwana ameniambia hivi, Katika muda wa mwaka, kama miaka ya mtu mwenye kuajiriwa, utaangamia utukufu wote wa Kedari. 17#Hes 23:19; 1 Sam 15:29; Isa 1:20; Mt 24:35; Mk 13:31; Lk 21:33; 1 Pet 1:25Na mabaki ya hesabu ya wavuta pinde, hao mashujaa wa Kedari watakuwa wachache; maana BWANA, Mungu wa Israeli, amenena neno hili.

Iliyochaguliwa sasa

Isa 21: SUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha