1 Fal 15:32-34
1 Fal 15:32-34 SUV
Kulikuwa na vita kati ya Asa na Baasha mfalme wa Israeli siku zao zote. Katika mwaka wa tatu wa Asa mfalme wa Yuda, Baasha mwana wa Ahiya alianza kutawala juu ya Israeli wote huko Tirza, akatawala miaka ishirini na minne. Akafanya yaliyo mabaya machoni pa BWANA akaiendea njia ya Yeroboamu, na kosa lake ambalo kwa hilo aliwakosesha Israeli.