Zaburi 82
82
Zaburi 82
Maombi kwa ajili ya kutaka haki
Zaburi ya Asafu.
1 Mungu anaongoza kusanyiko kuu,
anatoa hukumu miongoni mwa “miungu”:
2 “Hata lini utaendelea kuwatetea wasio haki
na kuonesha upendeleo kwa waovu?
3 Teteeni wanyonge na yatima,
tunzeni haki za maskini na waliodhulumiwa.
4Mwokoeni mnyonge na mhitaji,
wakomboeni kutoka mkononi mwa mwovu.
5 “Hawajui lolote, hawaelewi lolote.
Wanatembea gizani;
misingi yote ya dunia imetikisika.
6 “Nilisema, ‘Ninyi ni “miungu”;
ninyi nyote ni wana wa Aliye Juu Sana.’
7 Lakini mtakufa kama wanadamu wa kawaida;
mtaanguka kama mtawala mwingine yeyote.”
8 Ee Mungu, inuka uihukumu nchi,
kwa kuwa mataifa yote ni urithi wako.
Iliyochaguliwa sasa
Zaburi 82: NEN
Kuonyesha
Nakili
Linganisha
Shirikisha
Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia
Holy Bible, Kiswahili Contemporary Version™ (Neno: Biblia Takatifu™) | Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 by Biblica, Inc. | Used with permission. All rights reserved worldwide.
Biblica® Cross Reference System | Copyright © 2025 by Biblica, Inc. | Used with permission. All rights reserved worldwide.