Zaburi 67
67
Zaburi 67
Mataifa wahimizwa kumsifu Mungu
Kwa mwimbishaji. Na ala za nyuzi za muziki. Zaburi. Wimbo.
1 Mungu aturehemu na kutubariki,
na kutuangazia nuru za uso wake,
2 ili njia zako zijulikane duniani,
wokovu wako katikati ya mataifa yote.
3 Ee Mungu, mataifa na wakusifu,
mataifa yote na wakusifu.
4 Mataifa yote wafurahi na kuimba kwa shangwe,
kwa kuwa unatawala watu kwa haki
na kuongoza mataifa ya dunia.
5 Ee Mungu, mataifa na wakusifu,
mataifa yote na wakusifu.
6 Ndipo nchi itatoa mazao yake,
naye Mungu, Mungu wetu, atatubariki.
7 Mungu atatubariki
na miisho yote ya dunia itamcha yeye.
Iliyochaguliwa sasa
Zaburi 67: NEN
Kuonyesha
Nakili
Linganisha
Shirikisha
Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia
Holy Bible, Kiswahili Contemporary Version™ (Neno: Biblia Takatifu™) | Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 by Biblica, Inc. | Used with permission. All rights reserved worldwide.
Biblica® Cross Reference System | Copyright © 2025 by Biblica, Inc. | Used with permission. All rights reserved worldwide.