Zaburi 54
54
Zaburi 54
Kuomba ulinzi wa Mungu kutokana na adui
Kwa mwimbishaji. Na ala za nyuzi za uimbaji. Utenzi wa Daudi. Wakati Wazifu walimwendea Sauli na kumjulisha, “Je, Daudi hajifichi miongoni mwetu?”
1Ee Mungu uniokoe kwa jina lako,
unifanyie hukumu kwa uwezo wako.
2Ee Mungu, sikia maombi yangu,
usikilize maneno ya kinywa changu.
3Wageni wananishambulia,
watu wakatili wanayatafuta maisha yangu,
watu wasiomjali Mungu.
4Hakika Mungu ni msaada wangu,
Bwana ndiye anayenitegemeza.
5Mabaya na yawarudie wale wanaonisingizia,
kwa uaminifu wako uwaangamize.
6Nitakutolea dhabihu za hiari;
Ee Bwana, nitalisifu jina lako
kwa kuwa ni vyema.
7Kwa maana ameniokoa katika shida zangu zote,
na macho yangu yamewatazama adui zangu kwa ushindi.
Iliyochaguliwa sasa
Zaburi 54: NENO
Kuonyesha
Shirikisha
Nakili
Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia
Neno: Biblia Takatifu™ Neno™
Hakimiliki © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 na Biblica, Inc.
Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote.
Kiswahili Contemporary Version™
Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 by Biblica, Inc.
Used with permission. All rights reserved worldwide.