Zaburi 54
54
Zaburi 54
Kuomba ulinzi wa Mungu kutokana na adui
Kwa mwimbishaji. Na ala za nyuzi za uimbaji. Utenzi wa Daudi. Wakati Wazifu walimwendea Sauli na kumjulisha, “Je, Daudi hajifichi miongoni mwetu?”
1 Ee Mungu uniokoe kwa jina lako,
unifanyie hukumu kwa uwezo wako.
2 Ee Mungu, sikia maombi yangu,
usikilize maneno ya kinywa changu.
3 Wageni wananishambulia,
watu wakatili wanayatafuta maisha yangu,
watu wasiomjali Mungu.
4 Hakika Mungu ni msaada wangu,
Bwana ndiye anayenitegemeza.
5 Mabaya na yawarudie wale wanaonisingizia,
kwa uaminifu wako uwaangamize.
6 Nitakutolea dhabihu za hiari;
Ee Bwana, nitalisifu jina lako
kwa kuwa ni vyema.
7Kwa maana ameniokoa katika shida zangu zote,
na macho yangu yamewatazama adui zangu kwa ushindi.
Iliyochaguliwa sasa
Zaburi 54: NEN
Kuonyesha
Nakili
Linganisha
Shirikisha
Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia
Holy Bible, Kiswahili Contemporary Version™ (Neno: Biblia Takatifu™) | Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 by Biblica, Inc. | Used with permission. All rights reserved worldwide.
Biblica® Cross Reference System | Copyright © 2025 by Biblica, Inc. | Used with permission. All rights reserved worldwide.