Zaburi 41
41
Zaburi 41
Maombi ya mtu mgonjwa
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.
1Heri mtu yule anayemjali mnyonge,
Bwana atamwokoa wakati wa shida.
2 Bwana atamlinda na kuyahifadhi maisha yake,
atambariki katika nchi
na hatamwacha katika tamaa ya adui zake.
3 Bwana atamtegemeza akiwa mgonjwa kitandani,
na atamwinua kutoka kitandani mwake.
4Nilisema, “Ee Bwana nihurumie,
niponye, maana nimekutenda dhambi wewe.”
5Adui zangu wanasema kwa hila,
“Lini atakufa, na jina lake litokomee kabisa.”
6Kila anapokuja mtu kunitazama,
huzungumza uongo,
huku moyo wake ukikusanya masingizio;
kisha huondoka na kuyasambaza.
7Adui zangu wote hunongʼonezana dhidi yangu,
hao huniwazia mabaya sana, wakisema,
8“Ugonjwa mbaya sana umempata,
kamwe hatainuka tena kitandani mwake.”
9Hata rafiki yangu wa karibu niliyemwamini,
yule aliyekula chakula changu
ameniinulia kisigino chake.
10Lakini wewe, Ee Bwana, nihurumie,
ukaniinue tena, ili niweze kuwalipiza kisasi.
11Najua kwamba wapendezwa nami,
kwa kuwa adui yangu hanishindi.
12Katika uadilifu wangu unanitegemeza
na kuniweka kwenye uwepo wako milele.
13Mtukuzeni Bwana, Mungu wa Israeli,
tangu milele na hata milele.
Amen na Amen.
Iliyochaguliwa sasa
Zaburi 41: NENO
Kuonyesha
Shirikisha
Nakili

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia
Neno: Biblia Takatifu™ Neno™
Hakimiliki © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 na Biblica, Inc.
Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote.
Kiswahili Contemporary Version™
Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 by Biblica, Inc.
Used with permission. All rights reserved worldwide.