Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 29

29
Zaburi 29
Sauti ya Bwana wakati wa dhoruba
Zaburi ya Daudi.
1Mpeni Bwana, enyi mashujaa,
mpeni Bwana utukufu na nguvu.
2Mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake;
mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake.
3Sauti ya Bwana iko juu ya maji;
Mungu wa utukufu hupiga radi,
Bwana hupiga radi juu ya maji makuu.
4Sauti ya Bwana ina nguvu;
sauti ya Bwana ni tukufu.
5Sauti ya Bwana huvunja mierezi;
Bwana huvunja vipande vipande
mierezi ya Lebanoni.
6Hufanya Lebanoni irukaruke kama ndama,
Sirioni#29:6 yaani Mlima Hermoni urukaruke kama mwana nyati.
7Sauti ya Bwana hupiga
kwa miali ya radi.
8Sauti ya Bwana hutikisa jangwa;
Bwana hutikisa Jangwa la Kadeshi.
9Sauti ya Bwana huzalisha ayala,
na huuacha msitu wazi.
Hekaluni mwake wote wasema,
“Utukufu!”
10 Bwana huketi akiwa ametawazwa juu ya gharika;
Bwana ametawazwa kuwa Mfalme milele.
11 Bwana huwapa watu wake nguvu;
Bwana huwabariki watu wake kwa kuwapa amani.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 29: NENO

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia