Zaburi 125
125
Zaburi 125
Usalama wa watu wa Mungu
Wimbo wa kwenda juu.
1Wale wamtumainio Bwana ni kama Mlima Sayuni,
ambao hauwezi kutikisika, bali wadumu milele.
2Kama milima inavyozunguka Yerusalemu,
ndivyo Bwana anavyowazunguka watu wake
sasa na hata milele.
3Fimbo ya waovu haitadumu juu ya nchi
waliyopewa wenye haki,
ili wenye haki wasije wakatumia
mikono yao kutenda ubaya.
4Ee Bwana, watendee mema walio wema,
wale walio wanyofu wa moyo.
5Bali wale wanaogeukia njia zilizopotoka,
Bwana atawafukuza pamoja na watenda maovu.
Amani iwe juu ya Israeli.
Iliyochaguliwa sasa
Zaburi 125: NENO
Kuonyesha
Shirikisha
Nakili

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia
Neno: Biblia Takatifu™ Neno™
Hakimiliki © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 na Biblica, Inc.
Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote.
Kiswahili Contemporary Version™
Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 by Biblica, Inc.
Used with permission. All rights reserved worldwide.