Zaburi 124
124
Zaburi 124
Shukrani kwa ukombozi wa Israeli
Wimbo wa kwenda juu. Wa Daudi.
1Kama Bwana hangekuwa upande wetu;
Israeli na aseme sasa:
2kama Bwana hangekuwa upande wetu,
watu walipotushambulia,
3hasira yao ilipowaka dhidi yetu,
wangetumeza tukiwa hai,
4mafuriko yangegharikisha,
maji mengi yangetufunika,
5maji yaendayo kasi
yangetuchukua.
6Ahimidiwe Bwana,
ambaye hakuruhusu turaruliwe kwa meno yao.
7Tumeponyoka kama ndege
kutoka mtego wa mwindaji;
mtego umevunjika,
nasi tumeokoka.
8Msaada wetu ni katika jina la Bwana,
Muumba wa mbingu na dunia.
Iliyochaguliwa sasa
Zaburi 124: NENO
Kuonyesha
Shirikisha
Nakili

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia
Neno: Biblia Takatifu™ Neno™
Hakimiliki © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 na Biblica, Inc.
Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote.
Kiswahili Contemporary Version™
Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 by Biblica, Inc.
Used with permission. All rights reserved worldwide.