Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 119:17-48

Zaburi 119:17-48 NENO

Mtendee mema mtumishi wako, nami nitaishi; nitalitii neno lako. Yafungue macho yangu nipate kuona mambo ya ajabu katika sheria yako. Mimi ni mgeni duniani, usinifiche amri zako. Nafsi yangu inataabika kwa shauku kubwa kwa sheria zako wakati wote. Unawakemea wenye majivuno, waliolaaniwa, wanaoenda mbali na amri zako. Niondolee dharau na dhihaka, kwa kuwa ninazishika sheria zako. Ingawa watawala huketi pamoja na kunisingizia, mtumishi wako atatafakari juu ya maagizo yako. Sheria zako ni furaha yangu, nazo ni washauri wangu. BWANA Nimelazwa chini mavumbini, yahifadhi maisha yangu sawasawa na neno lako. Nilikueleza njia zangu ukanijibu, nifundishe sheria zako. Nijulishe mafundisho ya mausia yako, nami nitatafakari maajabu yako. Nafsi yangu imechakazwa kwa huzuni, uniimarishe sawasawa na neno lako. Niepushe na njia za udanganyifu, kwa neema unifundishe sheria zako. Nimechagua njia ya kweli, nimekaza moyo wangu katika sheria zako. Nimengʼangʼania sheria zako, Ee BWANA, usiniache niaibishwe. Nakimbilia katika njia ya maagizo yako, kwa kuwa umeuweka moyo wangu huru. Ee BWANA, nifundishe kuyafuata maagizo yako, nami nitayashika hadi mwisho. Nipe ufahamu, nami nitaishika sheria yako na kuitii kwa moyo wangu wote. Niongoze kwenye njia ya amri zako, kwa kuwa huko napata furaha. Ugeuze moyo wangu kuelekea sheria zako, na siyo kwenye mambo ya ubinafsi. Geuza macho yangu kutoka mambo yasiyofaa, uyahifadhi maisha yangu sawasawa na neno lako. Mtimizie mtumishi wako ahadi yako, ili upate kuogopwa. Niondolee aibu ninayoiogopa, kwa kuwa sheria zako ni njema. Tazama jinsi ninavyoonea shauku mausia yako! Hifadhi maisha yangu katika haki yako. BWANA Ee BWANA, upendo wako usiokoma unijie, wokovu wako sawasawa na ahadi yako, ndipo nitakapomjibu anayenidhihaki, kwa kuwa ninalitumainia neno lako. Usilinyakue neno la kweli kutoka kinywani mwangu, kwa kuwa nimeweka tumaini langu katika amri zako. Nitaitii amri yako daima, naam, milele na milele. Nitatembea huru, kwa kuwa nimejifunza mausia yako. Nitasema sheria zako mbele za wafalme wala sitaaibishwa, kwa kuwa ninazifurahia amri zako kwa sababu ninazipenda. Ninaziinulia amri zako ambazo ninazipenda mikono yangu, nami ninatafakari juu ya maagizo yako.