Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 119:153-160

Zaburi 119:153-160 NEN

Yaangalie mateso yangu, uniokoe, kwa kuwa sijasahau sheria yako. Nitetee katika hali hii yangu na unikomboe, uyahifadhi maisha yangu sawasawa na ahadi yako. Wokovu uko mbali na waovu, kwa kuwa hawatafuti maagizo yako. Ee BWANA, huruma zako ni kuu, uyahifadhi maisha yangu sawasawa na sheria zako. Adui wanaonitesa ni wengi, lakini mimi sitaziacha sheria zako. Ninawatazama wasioamini kwa chuki, kwa kuwa hawalitii neno lako. Tazama jinsi ninavyopenda mausia yako; Ee BWANA, uyahifadhi maisha yangu, sawasawa na upendo wako. Maneno yako yote ni kweli, sheria zako zote za haki ni za milele.

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha