Zaburi 115:1-11
Zaburi 115:1-11 NENO
Sio kwetu sisi, Ee BWANA, sio kwetu sisi, bali utukufu ni kwa jina lako, kwa sababu ya upendo na uaminifu wako. Kwa nini mataifa waseme, “Yuko wapi Mungu wao?” Mungu wetu yuko mbinguni, naye hufanya lolote limpendezalo. Lakini sanamu zao ni za fedha na dhahabu, zilizotengenezwa kwa mikono ya wanadamu. Zina vinywa, lakini haziwezi kusema, zina macho, lakini haziwezi kuona; zina masikio, lakini haziwezi kusikia, zina pua, lakini haziwezi kunusa; zina mikono, lakini haziwezi kupapasa, zina miguu, lakini haziwezi kutembea; wala koo zao haziwezi kutoa sauti. Wale wanaozitengeneza watafanana nazo, vivyo hivyo wale wote wanaozitumainia. Ee nyumba ya Israeli, mtumainini BWANA, yeye ni msaada na ngao yao. Ee nyumba ya Haruni, mtumainini BWANA, yeye ni msaada na ngao yao. Ninyi mnaomcha, mtumainini BWANA, yeye ni msaada na ngao yao.