Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 111

111
Zaburi 111#111 Zaburi hii imetungwa kila mstari ukianzia na herufi ya alfabeti ya Kiebrania zikifuatana tangu Aleph (A) hadi Taw (T); zote ni 22.
Sifa za Bwana kwa matendo ya ajabu
1Msifuni Bwana.#111:1 Msifuni Bwana kwa Kiebrania ni Hallelu Yah.
Nitamtukuza Bwana kwa moyo wangu wote,
katika baraza la wanyofu na katika kusanyiko.
2Kazi za Bwana ni kuu,
wote wanaopendezwa nazo huzitafakari.
3Kazi zake zimejaa fahari na utukufu,
haki yake hudumu daima.
4Amefanya maajabu yake yakumbukwe,
Bwana ni mwenye neema na huruma.
5Huwapa chakula wale wanaomcha,
hulikumbuka agano lake milele.
6Amewaonesha watu wake uwezo wa kazi zake,
akiwapa nchi za mataifa mengine.
7Kazi za mikono yake ni za uaminifu na haki,
mausia yake yote ni ya kuaminika.
8Zinadumu milele na milele,
zikifanyika kwa uaminifu na unyofu.
9Aliwapa watu wake ukombozi,
aliamuru agano lake milele:
jina lake ni takatifu na la kuogopwa.
10Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima,
wote wanaozifuata amri zake wana busara.
Sifa zake zadumu milele.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 111: NENO

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia