Zaburi 100
100
Zaburi 100
Dunia yote yaitwa kumsifu Mungu
Zaburi ya shukrani.
1 Mpigieni Bwana kelele za shangwe, dunia yote.
2 Mwabuduni Bwana kwa furaha;
njooni mbele zake kwa nyimbo za shangwe.
3 Jueni kwamba Bwana ndiye Mungu.
Yeye ndiye alituumba, sisi tu mali yake;
sisi tu watu wake,
kondoo wa malisho yake.
4 Ingieni malangoni mwake kwa shukrani
na katika nyua zake kwa kusifu,
mshukuruni yeye na kulisifu jina lake.
5 Kwa maana Bwana ni mwema
na fadhili zake zadumu milele;
uaminifu wake unadumu kwa vizazi vyote.
Iliyochaguliwa sasa
Zaburi 100: NEN
Kuonyesha
Nakili
Linganisha
Shirikisha
Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia
Holy Bible, Kiswahili Contemporary Version™ (Neno: Biblia Takatifu™) | Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 by Biblica, Inc. | Used with permission. All rights reserved worldwide.
Biblica® Cross Reference System | Copyright © 2025 by Biblica, Inc. | Used with permission. All rights reserved worldwide.