Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 1

1
KITABU CHA KWANZA
(Zaburi 1–41)
Zaburi 1
Furaha Ya Kweli
1 Heri mtu yule ambaye
haendi katika shauri la watu waovu,
wala hasimami katika njia ya wenye dhambi,
au kuketi katika baraza la wenye mizaha.
2 Bali huifurahia sheria ya Bwana,
naye huitafakari hiyo sheria usiku na mchana.
3 Mtu huyo ni kama mti uliopandwa
kando ya vijito vya maji,
ambao huzaa matunda kwa majira yake
na majani yake hayanyauki.
Lolote afanyalo hufanikiwa.
Huzuni Ya Waovu
4 Sivyo walivyo waovu!
Wao ni kama makapi
yapeperushwayo na upepo.
5 Kwa hiyo waovu hawatastahimili hukumu,
wala wenye dhambi katika kusanyiko la wenye haki.
6Kwa maana Bwana huziangalia njia za mwenye haki,
bali njia ya waovu itaangamia.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 1: NEN

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha