Hesabu 21:1-3
Hesabu 21:1-3 NENO
Mfalme wa Aradi, aliyekuwa Mkanaani aliyeishi huko Negebu, aliposikia kwamba Waisraeli walikuwa wanakuja kwa njia ya Atharimu, aliwashambulia Waisraeli na kuwateka baadhi yao. Ndipo Israeli akaweka nadhiri hii kwa BWANA: “Ikiwa utawatia watu hawa mikononi mwetu, tutaiangamiza kabisa miji yao.” BWANA akasikiliza ombi la Waisraeli, naye akawapa ushindi juu ya Wakanaani. Wakawaangamiza kabisa na miji yao; hivyo mahali pale pakaitwa Horma.